

Lugha Nyingine
Sudan Kusini yaanzisha mradi wa dola za kimarekani milioni 58 kuendeleza watoto shuleni
Sudan Kusini imeanzisha mradi wa miaka minne wa kuhimiza upatikanaji wa elimu bora na jumuishi na kuboresha matokeo ya mafunzo kwa ajili ya watoto haswa wa kike na wanaoishi katika mazingira duni.
Mradi huo uliofadhiliwa na Mfuko wa Ushirikiano wa Kimataifa kwa Elimu (GPE) utatekelezwa kwa pamoja na serikali ya Sudan Kusini, Umoja wa Mataifa na mashirika ya misaada, na unatarajiwa kunufaisha watoto zaidi ya laki tatu moja kwa moja na wengine laki sita kwa njia isiyo ya moja kwa moja katika kaunti 20 nchini humo.
Waziri wa Elimu na Mafunzo wa Sudan Kusini Kuyok Abol Kuyok, amesema ufadhili huo utatoa nafasi za upatikanaji wa elimu inayohitajika kwa watoto walioathiriwa na migogoro inayoendelea nchini humo, huku akitoa wito kwa viongozi wa jumuiya ya kimataifa kuongeza misaada husika ili kudumisha mwelekeo huo.
Kituo cha mafunzo cha Bajiquan mkoani Hebei, China chakaribisha wanafunzi kutoka Russia
Picha: Mandhari ya mbuga katika majira ya joto mkoani Gansu, China
Bustani ya Kimataifa ya Pump Track ya Shenyang, China: Utambulisho Mpya wa Michezo Mjini
Ukumbi wa Kuutazama Mji wa “Kilele cha Tianjin” wa China wafunguliwa rasmi kwa umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma