Lugha Nyingine
Vikosi vya Marekani vyakuwa na "udhibiti kamili kabisa" juu ya anga ya Iran hivi karibuni

Msemaji wa Ikulu ya White House Karoline Leavitt akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari katika Ikulu ya White House mjini Washington, D.C., Marekani, Machi 4, 2026. (Picha na Li Yuanqing/Xinhua)
WASHINGTON – Msemaji wa Ikulu ya White House ya Marekani Karoline Leavitt amesema kwamba vikosi vya Marekani vitakuwa na "udhibiti kamili kabisa" juu ya anga ya Iran katika saa chache zijazo.
"Tunatarajia kuwa na udhibiti kamili kabisa juu ya anga ya Iran katika saa zijazo," Leavitt alisema Jumatano kwenye mkutano na waandishi wa habari wa siku katika Ikulu ya White House.
Aliongeza kuwa kupeleka wanajeshi wa ardhini wa Marekani nchini Iran hakuko kwenye mipango kwa sasa, ingawa Rais wa Marekani Donald Trump alisema mapema kwamba yuko wazi kwa chaguo hilo katika siku zijazo.
Mapema siku hiyo, Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth alisema kwenye mkutano uliofanyika katika makao makuu ya wizara ya ulinzi ya Marekani, Pentagon kwamba operesheni hiyo ya kijeshi kati ya Marekani na Israeli dhidi ya Iran bado iko katika hatua zake za mapema.
Dan Caine, mwenyekiti wa Wakuu wa Vikosi vya Majeshi ya Marekani, amesema vikosi vya Marekani vitaanza kushambulia kwa mfululizo ndani zaidi katika ardhi ya Iran wakati operesheni zikiendelea kupanuka.
Iran na kundi la wanamgambo wa Lebanon Hezbollah wamefanya mashambulizi yao ya kwanza yaliyoratibiwa dhidi ya Israeli huku kukiwa na kupamba moto kunakoendelea, Jeshi la Ulinzi la Israeli lilikiambia chombo cha habari cha CNN Jumatano.
Jumamosi asubuhi wiki iliyopita, mashambulizi ya anga ya Marekani na Israeli dhidi ya Iran yalimuua Kiongozi Mkuu wa Iran Ayatollah Ali Khamenei, pamoja na baadhi ya wanafamilia wa kiongozi huyo, makamanda waandamizi wa kijeshi na raia.
Iran ilijibu mapigo kupitia mawimbi ya mashambulizi ya makombora na droni zilizolenga Israeli na vituo vya kijeshi vya Marekani katika nchi mbalimbali za Mashariki ya Kati.

Sikukuu ya Jadi ya Taa ya China yasherehekea mkoani Zhejiang

Kupatwa kwa mwezi kikamilifu kwashuhudiwa katika sehemu mbalimbali nchini China

"Tamasha la Maolong" la kabila la Wayilao lasherehekewa kwa ngoma ya dragoni mkoani Guizhou, China

Mji mkongwe wa Wuzhen, China wazindua shughuli mbalimbali wakati wa Mwaka Mpya wa Jadi wa China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma