Kampuni za China zaangazia fursa za Afrika kwenye maonesho ya Hostex

(CRI Online) Machi 10, 2026

Kampuni za China zimeonesha mvuto mkubwa kwenye maonesho ya Hostex 2026 yanayoendelea jijini Johannesburg, Afrika Kusini, kwa bidhaa zao zilizovutia wafanyabiashara wengi kutafuta namna ya kufanya ushirikiano mpya wa kibiashara.

Yakiwa ni maonesho ya biashara ya chakula, vinywaji, na hoteli yanayoongoza barani Afrika, Hostex inawaleta pamoja wasambazaji, wanunuzi, na wataalamu wa sekta kutoka bara zima la Afrika. Yakiadhimisha miaka yake 40 mwaka huu, maonesho hayo yamevutia waoneshaji kutoka nchi nyingi.

Miongoni mwa washiriki wa kimataifa, kampuni za China zimejitokeza katika kumbi nyingi, zikionesha teknolojia mbalimbali za jikoni, mashine za kusindika chakula, na suluhu endelevu za vifungashio.

Wataalamu wa sekta wanaohudhuria maonesho hayo wameonesha matumaini yao kuhusu uhusiano huo unaopanuka. Jesline Musokomi, msambazaji kutoka Johannesburg, amesema wasambazaji wa China hutoa aina mbalimbali za bidhaa na huduma ambazo zinafungua milango kwa biashara ndogo na za kati kupata vifaa ambavyo vinginevyo vingekuwa ghali sana.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha