Tanzania kukarabati miundombinu iliyoharibiwa na mvua kubwa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti

(CRI Online) Machi 10, 2026

Waziri wa Maliasili na Utalii wa Tanzania Ashatu Kijaji ametangaza kuwa Tanzania itatenga shilingi bilioni 8.1 za Tanzania (dola za Marekani karibu milioni 3.2) kukarabati barabara na madaraja yaliyoharibiwa na mvua kubwa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti.

Hayo ameyasema Jumapili jioni wakati wa ziara ya ukaguzi wa hifadhi hiyo, ambapo alitathmini uharibifu uliosababishwa na mvua kubwa za hivi karibuni zinazohusiana na mabadiliko ya tabianchi, ambazo zimesababisha magari kadhaa ya watalii kukwama kwa muda mrefu.

Kijaji amesema serikali itatoa fedha hizo haraka ili kuhakikisha ukarabati wa miundombinu iliyoathiriwa unafanywa kwa wakati, ikiwa ni pamoja na madaraja na barabara muhimu kwa shughuli za utalii katika hifadhi hiyo.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha