Lugha Nyingine
Rais wa Tanzania atoa wito wa ulinzi wa Eneo la Urithi wa Dunia la Ngorongoro
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amesema Alhamisi wiki hii kuwa Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ni eneo la kipekee la urithi wa dunia ambalo lazima lilindwe kwa manufaa ya Tanzania na pia jumuiya ya kimataifa.
Rais Samia ameyasema hayo katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma, baada ya kupokea ripoti za tume mbili za serikali alizoziunda kufanya tathmini ya matumizi ya ardhi katika eneo hilo la Ngorongoro.
Ameelezea sifa za kipekee za mazingira ya asili za eneo hilo, ikiwemo Kreta maarufu ya Ngorongoro, ambayo ina kina cha urefu wa mita takriban 600 na inaunga mkono mfumo tajiri wa kiikolojia wa spishi za wanyamapori na ndege.
Pia amesisitiza umuhimu wa eneo hilo duniani kwa historia ya binadamu na utafiti wa kisayansi. Aidha, amesema hifadhi hiyo ina mazingira anuwai ya asili, yakiwemo savana, eneo la misitu na volkano, ambayo baadhi yao wanasayansi wanaamini bado yako hai.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



