Mkutano wa tabianchi wa Afrika wahimiza uwekezaji katika kilimo cha kisasa chenye kuhimili mabadiliko

(CRI Online) Machi 24, 2026

Mkutano wa tatu wa Biashara Duniani wa Mabadiliko ya Tabianchi juu ya Afrika umefunguliwa Jumatatu mjini Nairobi ukihimiza wawekezaji wa kimataifa kufadhili kilimo cha kisasa kinachohimili mabadiliko ya tabianchi, ili kuongeza usalama wa chakula barani Afrika.

Mkutano huo wa siku mbili umewaleta pamoja viongozi wa kimataifa, wadau wa sekta binafsi na wawekezaji, ili kuhimiza ufadhili wa tabianchi, utunzaji wa mazingira na mpito wa haki.

Waziri wa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo wa Kenya Bw. Mutahi Kagwe, ameonya kuwa kushindwa kufadhili kilimo cha kisasa kinachohimili mabadiliko ya tabianchi barani Afrika, kunaweza kusababisha madhara makubwa katika mifumo ya chakula duniani.

Bw. Kagwe amesema mabadiliko ya tabianchi tayari yanaathiri vibaya mifumo ya jadi ya kilimo kote nchini Kenya, huku mienendo ya hali kali kupitiliza za hewa sasa ikiwa ni hali halisi ya nchi hiyo.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha