Uungaji mkono kwa Trump wafikia kiwango kipya cha chini wakati wa malalamiko kwa bei za juu za mafuta na vita dhidi ya Iran

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 25, 2026

WASHINGTON – Makadirio ya kumkubali Rais wa Marekani Donald Trump yameshuka siku za hivi karibuni hadi kiwango cha chini kabisa tangu kuanza kwa muhula wake wa pili, kutokana na malalamiko ya watu wengi juu ya kupanda kwa bei za mafuta na vita alivyovianzisha dhidi ya Iran, kura ya maoni ya Reuters/Ipsos iliyotolewa jana Jumanne inaonesha.

Kura hiyo ya maoni iliyofanywa kwa siku nne na kukamilika Jumatatu, imebaini kuwa asilimia 36 ya raia wa Marekani wanakubali utendaji wa Trump, ikiwa ni kiwango cha chini kutoka asilimia 40 iliyorekodiwa katika kura ya maoni ya Reuters/Ipsos iliyofanyika wiki iliyopita.

Kura ya maoni ya hivi karibuni zaidi inaonyesha kuwa asilimia 25 tu ya waliohojiwa wanakubali namna Trump anavyoshughulikia gharama ya maisha -- suala muhimu ambalo Trump mwenyewe alijisifu kwa ushindi wake katika uchaguzi wa rais mwaka 2024.

Kura hiyo ya maoni imebaini kwamba, asilimia 29 pekee ya waliohojiwa wanakubali usimamizi wa uchumi wa Trump, ambacho ni kiwango cha chini kabisa kuhusu mafanikio yake ya kazi katika mihula ya Rais Trump, na ni kiwango cha chini kuliko kiwango chochote cha kukubali ufanisi katika uchumi kwa Rais wa zamani wa Marekani Joe Biden. Zaidi ya wiki tatu baada ya vita dhidi ya Iran, Trump anakabiliwa na madai ya kumtaka kukomesha mgogoro huo, madai ambayo yanazidi kuongezeka kutoka kwa washirika wake wa kisiasa, viongozi wa biashara na hata kambi yake ya MAGA ("Make America Great Again").

Viongozi kadhaa muhimu wa maoni wa MAGA wameelezea upingaji wao hadharani, akiwemo Steve Bannon, mwanamkakati mkuu wa zamani wa Trump, mtoa maelezo ya kisiasa Tucker Carlson, na mtangazaji wa vyombo vya habari Megyn Kelly.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha