Lugha Nyingine
Spika wa Bunge la China akutana na wageni kutoka Azerbaijan, Kazakhstan, wajumbe wa bodi ya wakurugenzi ya BFA

Zhao Leji, Spika wa Bunge la Umma la China, akikutana na Spika wa Bunge la Taifa (Milli Majlis) la Azerbaijan Sahiba Gafarova, ambaye yuko China kwa ajili ya Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia (BFA) 2026, Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China, Machi 25, 2026. (Xinhua/Li Tao)
BOAO, Hainan – Spika wa Bunge la Umma la China Zhao Leji alikutana jana Jumatano kwa nyakati tofauti na Spika wa Bunge la Taifa (Milli Majlis) la Azerbaijan Sahiba Gafarova na Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza wa Kazakhstan Roman Sklyar, ambao wako Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China, kwa kushiriki kwenye Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia (BFA) 2026.
Zhao, mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la Umma la China (NPC) pia alikutana na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi na washauri wakuu wa BFA siku hiyo ya Jumatano.
Katika mkutano wake na Gafarova, Zhao amesema kwamba China iko tayari kushirikiana na Azerbaijan kufuata maafikiano muhimu yaliyofikiwa na viongozi wawili wa nchi hizo, kupanua ushirikiano wa kiuchumi, biashara na uwekezaji, kuongeza muunganisho, kuhimiza mawasiliano ya kati ya watu na watu, na kwa pamoja kusukuma mbele ujenzi wa jumuiya yenye mustakabali wa pamoja wa binadamu.
Gafarova amesema Azerbaijan inashikilia kithabiti kanuni ya kuwepo kwa China moja na ipo tayari kuimarisha ushirikiano na China katika nyanja mbalimbali na kuongeza kwa kina mawasiliano kati ya vyombo vya kutunga sheria vya nchi hizo mbili.
Alipokutana na Sklyar, Zhao amebainisha kuwa China na Kazakhstan ni majirani marafiki na washirika wa kudumu wa kimkakati wa pande zote.
Zhao amesema China iko tayari kushirikiana na Kazakhstan kutekeleza maafikiano muhimu yaliyofikiwa na viongozi wa nchi hizo mbili, kuimarisha kuaminiana kisiasa, kuongeza kwa kina ushirikiano wa kivitendo huku ushirikiano wa kiwango cha juu wa Ukanda Mmoja, Njia Moja ukiwa ni kipaumbele.
Sklyar amesema Kazakhstan inaunga mkono mapendekezo ya kimataifa yaliyotolewa na China, na ameongeza kuwa uhusiano kati ya Kazakhstan na China umekuwa ukiendelea kuwa wa kina zaidi, na kwamba Kazakhstan ina nia ya kuimarisha ushirikiano na China katika nyanja mbalimbali kama vile utungaji wa sheria, uchumi, biashara na nishati ili kuhimiza maendeleo ya uhusiano wa pande mbili.
Alipokutana na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi na washauri wakuu wa BFA, Zhao amesema China iko tayari kushirikiana na pande zote ili kutekeleza kwa pamoja mapendekezo ya kimataifa na kuhimiza ujenzi wa jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja.
Mwenyekiti wa BFA Ban Ki-moon na wawakilishi wengine wamesifu maono ya kujenga jumuiya ya binadamu yenye mustakabali wa pamoja na mapendekezo ya kimataifa yaliyotolewa na China, wakielezea nia yao ya kufanya juhudi zisizokoma ili kuhimiza maendeleo ya jukwaa hilo.

Zhao Leji, mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la Umma la China, akikutana na Spika wa Bunge la Taifa (Milli Majlis) la Azerbaijan Sahiba Gafarova, ambaye yuko China kwa ajili ya Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia (BFA) 2026, Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China, Machi 25, 2026. (Xinhua/Li Tao)

Zhao Leji, mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la Umma la China, akikutana na Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza wa Kazakhstan Roman Sklyar, ambaye yuko China kwa ajili ya Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia (BFA) 2026, Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China, Machi 25, 2026. (Xinhua/Shen Hong)

Zhao Leji, mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la Umma la China, akikutana na Naibu Waziri Mkuu wa Kwanza wa Kazakhstan Roman Sklyar, ambaye yuko China kwa ajili ya Mkutano wa Mwaka wa Jukwaa la Boao la Asia (BFA) 2026, Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China, Machi 25, 2026. (Xinhua/Shen Hong)

Zhao Leji, mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge la Umma la China, akikutana na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi na washauri wakuu wa Jukwaa la Boao la Asia (BFA), Boao, Mkoa wa Hainan, kusini mwa China, Machi 25, 2026. (Xinhua/Shen Hong)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



