Trump "ana nia hasa" ya kuziomba nchi za Kiarabu kusaidia kugharamia vita vya Marekani na Israeli dhidi ya Iran: Ikulu ya Marekani

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 31, 2026

WASHINGTON – Msemaji wa Ikulu ya Marekani White House Karoline Leavitt amesema kuwa Rais wa Marekani Donald Trump "atakuwa na nia hasa" katika kuwataka nchi za Kiarabu kusaidia kulipia gharama zinazohusiana na vita vinavyoendelea vya Marekani na Israeli dhidi ya Iran.

"Sitamtangulia (Trump) kuhusu hilo," Leavitt amesema kwenye mkutano na waandishi wa habari wa Ikulu ya Marekani jana Jumatatu. "Lakini hakika ni wazo ambalo najua analo na jambo ambalo nadhani mtalisikia zaidi kutoka kwake."

Maafisa wa Makao Makuu ya Wizara ya Ulinzi ya Marekani, Pentagon, waliliambia Bunge la Marekani mapema mwezi huu kwamba utawala wa Trump ulitumia dola za Marekani zaidi ya bilioni 11.3 katika siku sita za kwanza za vita vyake dhidi ya Iran.

Kiasi hicho hakijumuishi uharibifu wa vita na fidia kwa hasara, ambavyo huenda vimeigharimu Pentagon dola za Marekani takriban bilioni 1.4 hadi bilioni 2.9 katika wiki tatu za kwanza za vita hivyo, kwa mujibu wa ripoti ya Jarida la Wall Street, ikimnukuu Elaine McCusker, afisa wa zamani wa bajeti wa Pentagon ambaye amekuwa akifuatilia gharama hizo kwa niaba ya Taasisi ya Biashara ya Marekani.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha