Je, 'gawio la idadi ya watu' la China limetoweka?

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 31, 2026

(Mchoraji: Xia Qing/GT)

(Mchoraji: Xia Qing/GT)

Kadri mabadiliko mapya yanapoibuka katika muundo wa umri wa idadi ya watu wa China, baadhi ya watoa maoni wa nchi za Magharibi wanadai kwamba maendeleo ya siku za baadaye ya China yatapoteza "kasi yake ya mgawanyiko wa idadi ya watu kwa rika." Madai ya namna hiyo si tu yanapuuza kanuni za msingi za maendeleo ya idadi ya watu lakini pia yanaonyesha uelewa mbaya na maoni yenye makosa kuhusu mantiki iliyo nyuma ya maendeleo yenye sifa bora ya idadi ya watu ya China.

Masuala ya idadi ya watu si swali rahisi la ”ama-au”, kama dhana isemavyo: "watu wachache humaanisha ukuaji wa polepole zaidi; wazee zaidi humaanisha mizigo mizito zaidi." Kwa mujibu wa nadharia ya kiuchumi, nguvu kazi kama jambo la uzalishaji huathiri maendeleo ya kiuchumi kupitia vyote idadi yake na ubora wake.

Takwimu zinaonyesha kwamba wastani wa miaka ya kusoma shuleni kwa wastaafu wenye umri wa miaka karibu 60 nchini China ni kama miaka saba hadi minane, huku wastani wa miaka hiyo kwa vijana wanaoingia soko la ajira kwa mara ya kwanza ukifikia miaka 14. Hii ina maana kwamba ongezeko la nguvukazi yenye ufanisi linalochangiwa na wafanyakazi wapya linazidi kwa mbali punguzo linalosababishwa na kustaafu, hali ambayo inasababisha ukuaji wa jumla wa nguvukazi yenye ufanisi. China sasa inapitia mabadiliko kutoka "gawio la idadi ya watu" hadi "gawio la vipaji." Hadi kufikia mwisho wa 2025, idadi ya jumla ya watu wa China ilibaki kuwa kubwa katika bilioni 1.405, ikiwa na watu milioni 851 wenye umri wa kufanya kazi (16-59).

Kiwango cha nguvu kazi yake kinazidi nguvu kazi ya pamoja ya nchi zenye uchumi mkubwa ulioendelea barani Ulaya na Marekani, kikiwa miongoni mwa vikubwa zaidi duniani na kikitumika kama msingi imara wa maendeleo ya kiuchumi yenye sifa bora. Wakati huo huo, soko kubwa la ndani linaloundwa na idadi hiyo kubwa ya watu, vilevile na mfumo jumuishi wa viwanda na rasilimali watu nyingi vinabaki kuwa nguzo muhimu inayowezesha uchumi wa China kuhimili mishtuko ya nje na kudumisha ukuaji tulivu.

Kadri ubora wa jumla wa idadi ya watu unavyoendelea kuimarika, faida bora ya China katika rasilimali watu inazidi kuwa dhahiri zaidi. Kiwango cha kitaifa cha udahiri wa jumla katika elimu ya juu kimeongezeka hadi asilimia zaidi ya 60, na wastani wa miaka ya kusoma shuleni miongoni mwa idadi ya watu wenye umri wa kufanya kazi umefikia miaka 11.3, sawa na kiwango cha mwaka wa pili wa chuo kikuu.

Zaidi ya asilimia 60 ya wafanyakazi wapya walioongezwa kwenye soko la ajira wamepokea elimu ya juu. Jumla ya watu wenye elimu ya juu imezidi milioni 250, kubwa zaidi duniani, na inaendelea kuongezeka kwa milioni zaidi ya 10 kila mwaka. Wakati huo huo, nguvu kazi inayozidi kuongezeka ya wataalamu wenye ujuzi wa hali ya juu, wenye taaluma mbalimbali inaibuka kuunga mkono maendeleo ya nguvu mpya za uzalishaji zenye sifa bora. China kwa sasa ina kundi kubwa zaidi la wataalamu wa utafiti na maendeleo duniani.

Uwezo mkubwa wa “uchumi wa silva” (uchumi wa wazee) uliojikita katika mchakato wa kuzeeka kwa idadi ya watu pia unakuwa chanzo kipya cha ukuaji kutokana na mgawanyiko wa idadi ya watu kwa rika. Hadi kufikia mwisho wa 2025, miongoni mwa idadi ya watu wa China wenye umri wa miaka 60 na zaidi, wale wenye umri wa miaka 60-69, ambao kwa ujumla ni wazee wenye afya njema na wanaoonekana vijana, walichukua asilimia zaidi ya 55, jumla ya watu zaidi ya milioni 150. Kundi hili la watu, wenye afya njema, ujuzi wa kitaaluma, uzoefu mwingi na nia kubwa ya kushiriki katika shughuli za kijamii, linawakilisha nyongeza muhimu kwa kundi la rasilimali watu la China, lenye uwezo mkubwa wa maendeleo zaidi. Wakati huo huo, kadri viwango vya mapato na mahitaji ya matumizi ya wazee vinavyozidi kuongezeka, "uchumi wa silva" umeibuka kuwa injini mpya ya ukuaji.

Sera za idadi ya watu za China hazijawahi kutegemea vipimo visivyobadilika au vya upande mmoja. Badala yake, zinawakilisha muundo wa kitaasisi wa kimfumo unaobadilishwa kulingana na mabadiliko ya idadi ya watu wakati huohuo zikiwianisha mahitaji ya haraka na malengo ya muda mrefu. Hii inaonyesha mbinu ya kisayansi ya usimamizi wa kisasa wa idadi ya watu.

Kipindi cha Mpango wa 15 wa Miaka Mitano kitakuwa hatua ya kina zaidi ya mabadiliko ya mgawanyiko wa idadi ya watu kwa rika wa China. Katika kukabiliana na changamoto duniani za kuzaliana kwa kiwango cha chini na kuzeeka kwa idadi ya watu, China inabaki kudhamiria katika kuingiza uhakika kwenye maendeleo duniani kupitia ukuaji wake wenye sifa bora.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha