Rais wa Afrika Kusini ataka fidia ya utumwa ili kukabiliana na deni na maendeleo ya Afrika

(CRI Online) Mei 05, 2026

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amerejea tena wito wake wa kutaka fidia ya utumwa wakati maadhimisho ya Mwezi wa Afrika yanapoanza katika bara hilo.

Katika jarida la habari lililotolewa jana jumatatu, Rais Ramaphosa amesema karne nyingi za unyonyaji na uporaji wa kimfumo wa rasilimali za Afrika zinaendelea kusababisha uharibifu wa kiuchumi unaoendelea kwa mataifa ya Afrika.

Amesema fidia lazima iwe zaidi ya malipo ya kifedha na ijumuishe kuongezeka kwa uwekezaji wa moja kwa moja wa kigeni na ufikiaji wa soko kwa nchi za Afrika zilizoathiriwa na utumwa.

Pia rais Ramaphosa ametaka uhamisho wa teknolojia na ujuzi, pamoja na kurudishwa bila ya masharti yoyote kwa vitu vya sanaa vilivyoibiwa kutoka bara hilo karne nyingi zilizopita.

(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)

Picha