Lugha Nyingine
Tanzania yapanua miundombinu ya bandari ya Dar es Salaam ili kuongeza uwezo na ufanisi
(CRI Online) Mei 14, 2026
Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania Bw. Makame Mbarawa amesema, serikali ya nchi hiyo inatekeleza miradi mikubwa ya miundombinu ili kupanua uwezo na ufanisi wa bandari ya Dar es Salaam wakati ambapo kiasi cha mzigo kikiendelea kuongezeka.
Akiwasilisha mapendekezo ya bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2026/2027 bungeni Dodoma, Bw. Mbarawa amesema serikali imechukua hatua thabiti kuboresha ushughulikiaji wa mizigo na kuimarisha nafasi ya Tanzania ya kuwa kituo cha biashara na ugavi cha kikanda.
Ameeleza kuwa serikali inasukuma mbele ujenzi wa reli ya SGR inayounganishwa kwenye bandari hiyo, pamoja na maendeleo ya yadi ya Malindi kwa ajili ya kupakia mizigo kwenye treni za mizigo za reli ya SGR.
(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)
Kuhusu Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



