Tanzania yazidisha utayari wa kukabiliana na Ebola wakati mlipuko wa DRC ukizua wasiwasi wa kikanda

(CRI Online) Mei 18, 2026

Tanzania imeongeza hatua za ufuatiliaji, uchunguzi wa mpakani na utayari wa kukabiliana na dharura kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Hayo yamesemwa jana Jumapili na Mkurugenzi wa Huduma za Dharura na Maafa kutoka Wizara ya Afya ya Tanzania, Erasto Sylvanus, akieleza kuwa serikali inafanya kazi kwa karibu na Shirika la Afya Duniani (WHO) na nchi jirani ili kuimarisha kinga, utambuzi wa mapema na mifumo ya kukabiliana kwa haraka na maambukizi dhidi ya uwezekano wowote wa kuingizwa kwa ugonjwa huo.

Amesema kwa ushirikiano na ofisi ya WHO nchini, Tanzania imefanya tathmini ya haraka ya ukaribu na mwingiliano na maeneo ya mlipuko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda ili kutambua maeneo yaliyo katika hatari kubwa na kuchukua hatua zinazofaa kwa mujibu wa Kanuni za Afya za Kimataifa.

Ameongeza kuwa timu za wataalamu katika ngazi ya kitaifa zimetumwa katika maeneo yenye hatari kubwa, huku timu za ziada zikiwa tayari kukabiliana na mahitaji yanayojitokeza.

(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)

Picha