Mgomo wa usafiri nchini Kenya wasimamishwa kwa ajili ya mazungumzo

(CRI Online) Mei 20, 2026

Kenya imetangaza kusimamishwa kwa mgomo wa usafiri wa umma kwa wiki moja jana Jumanne kufuatia maandamano ya kupinga ongezeko kubwa la bei ya mafuta yaliyosababisha vifo vya watu wanne.

Waziri wa Usalama wa Ndani wa Kenya, Onesimus Kipchumba Murkomen amesema kwamba usimamishaji huo kwa wiki moja utaruhusu serikali na wadau wa usafiri kuendelea na mashauriano.

“Serikali inaendelea kuwa na dhamira kikamilifu katika kushughulikia malalamiko yaliyotolewa na Wakenya wakati wote na inatoa wito wa njia za amani na kisheria za kuwasilisha malalamiko.” ameuambia mkutano wa pamoja na wanahabari jijini Nairobi.

Mgomo huo, ulioanza Jumatatu ukipinga kupanda kwa bei ya mafuta, ulivuruga usafiri wa umma na sekta ya elimu katika miji mikubwa nchini humo. Tangu kutolewa kwa tangazo hilo Muungano wa Sekta ya Uchukuzi, ambao uliitisha mgomo huo, umetoa wito kwa wanachama wake kuanza tena shughuli kote nchini.

(Wahariri wa tovuti:Zhao Jian)

Picha