Lugha Nyingine
Shindano la umahiri wa lugha ya Kichina lafanyika Rwanda

Nkurunziza Tharcisse, mshindi wa fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya "Daraja la Lugha ya Kichina" ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo, akipiga picha na Gao Wenqi, Balozi wa China nchini Rwanda, mjini Kigali, Rwanda, Mei 24, 2026. (Xinhua/Liu Youmin)
KIGALI - Fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya "Daraja la Lugha ya Kichina" ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo na Shule za Sekondari imefanyika Kigali, mji mkuu wa nchi hiyo, Jumapili.
Shindano hilo, lililoandaliwa na Ubalozi wa China nchini Rwanda na kuratibiwa na Taasisi ya Confucius katika Chuo Kikuu cha Rwanda, lilikusanya wanafunzi kutoka chuo hicho na wanafunzi kadhaa wa shule za sekondari wanaosoma lugha ya Kichina.
Gao Wenqi, Balozi wa China nchini Rwanda, amesisitiza kwamba Daraja la Lugha ya Kichina linaunganisha tamaduni za China na Rwanda, linaongeza ushirikiano wa kivitendo kati ya nchi hizo mbili, na kuimarisha uhusiano kati ya watu wa nchi hizo mbili.
Akibainisha kuwa nchini Rwanda, wanafunzi zaidi ya 20,000 wamejiunga na jumuiya ya kujifunza lugha ya Kichina, Gao amewahimiza washindi wa fainali hiyo kupata uelewa wa kina wa China kwa macho na mioyo yao, na kuwaelezea familia na marafiki zao kuhusu China halisi.
Eric Niyongabo, mratibu wa elimu wa kimkoa wa Kigali katika Wizara ya Elimu ya Rwanda, amesema kwamba mawasiliano ya kielimu na kitamaduni yanabaki kuwa nguzo muhimu ya ushirikiano kati ya Rwanda na China.
"Kupitia mipango kama vile Mashindano ya Daraja la Lugha ya Kichina, ufadhili wa masomo, ushirikiano wa kitaaluma, na ufanyaji kazi kwa pamoja wa kitaasisi, wanafunzi wetu wanapata kuonekana kimataifa na wanajiandaa kwa mustakabali uliounganishwa duniani," Niyongabo amebainisha.
Ubingwa wa shindano hilo kwa Wanafunzi wa Vyuo umechukuliwa na Nkurunziza Tharcisse kutoka Chuo cha Elimu cha Chuo Kikuu cha Rwanda, huku Gwiza Sabrina kutoka Ecole Notre Dame de la Providence de Karubanda akishinda taji hilo katika shindano hilo kwa wanafunzi wa shule za sekondari.
Kuanzia mwaka 2014 hadi 2026, Ubalozi wa China nchini Rwanda na Taasisi ya Confucius katika Chuo hicho wamefanikiwa kufanya Mashindano 13 ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya Daraja la Lugha ya Kichina kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari na Mashindano 12 ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya Daraja la Lugha ya Kichina kwa Wanafunzi wa Vyuo nchini Rwanda.

Gwiza Sabrina, mshindi wa fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya Daraja la Lugha ya Kichina ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Shule za Sekondari nchini Rwanda, akitoa hotuba kwenye shindano hilo mjini Kigali, Rwanda, Mei 24, 2026. (Xinhua/Liu Youmin)

Wapenda lugha ya Kichina wakitazama fainali ya Rwanda ya Mashindano ya Umahiri wa Lugha ya Kichina ya Daraja la Lugha ya Kichina ya mwaka 2026 kwa Wanafunzi wa Vyuo na Shule za Sekondari nchini Rwanda, mjini Kigali, Rwanda, Mei 24, 2026. (Xinhua/Liu Youmin)
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



