Iran yataka kuondolewa kwa kizuizi cha bandari zake ili kurejesha upitaji wa meli kwenye mlango wa Hormuz

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Mei 28, 2026

Watu wakishiriki kwenye tukio la ukumbusho lililofanyika kuomboleza wanafunzi wa shule ya msingi waliouawa katika shambulio la kombora kusini mwa Iran, Tehran, Iran, Aprili 7, 2026. (Xinhua/Shadati)

Watu wakishiriki kwenye tukio la ukumbusho lililofanyika kuomboleza wanafunzi wa shule ya msingi waliouawa katika shambulio la kombora kusini mwa Iran, Tehran, Iran, Aprili 7, 2026. (Xinhua/Shadati)

TEHRAN - Iran ina mswada wa mfumo wa awali na usio rasmi wa makubaliano (MoU) na Marekani, ambayo inataka kuondolewa kwa jeshi la Marekani na kizuizi cha Kikosi cha Majini cha Jeshi la nchi hiyo kwenye bandari zake, vyombo kadhaa vya habari vimeripoti jana Jumatano, vikirejelea ripoti ya IRIB TV ya serikali ya Iran.

Kwa kubadilishana na hilo, Iran imeahidi kurejesha usafiri wa meli za kibiashara kupitia Mlango-Bahari wa Hormuz hadi viwango vya kabla ya vita ndani ya mwezi mmoja na kudhibiti safari za meli kupitia mlango-bahari huo na Oman, ripoti hizo zimesema, zikiongeza kuwa meli za kijeshi hazijajumuishwa kwenye makubaliano.

Kwa mujibu wa ripoti hizo, Marekani imekubali kuondoa kizuizi chake cha kikosi cha majini kwenye bandari za Iran, kutambua usimamizi wa Iran wa usafiri wa baharini kupitia Mlango-Bahari wa Hormuz kwa ushirikiano na Oman, kukubali njia zilizoteuliwa na Iran za kupitisha meli, na kuondoa vikosi vya Marekani kutoka maeneo yanayozunguka Iran.

Zimesema, makubaliano yoyote ya mwisho kati ya Marekani na Iran yaliyofikiwa ndani ya kipindi cha mazungumzo cha siku 60 yataidhinishwa kwa njia ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lenye nguvu ya kisheria pande husika.

Chini ya makubaliano hayo, Iran haitachukua hatua yoyote bila "uthibitisho dhahiri," ripoti hizo zimeongeza.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Esmaeil Baghaei alithibitisha Jumamosi kwamba Iran na Marekani zinafanya kazi kukamilisha MoU hiyo ya kukomesha vita.

"Nia yetu imekuwa kwanza kukubaliana juu ya MoU yenye vifungu 14," Baghaei aliiambia IRIB TV, akiongeza kuwa pande hizo mbili zililenga kufikia makubaliano ya mwisho "ndani ya kipindi cha siku 30 hadi 60" yakihusu masuala kama vile kukomesha mashambulizi ya baharini ya Marekani na kuachiliwa kwa mali za Iran zinazozuiliwa.

Iran, Marekani, na Israel zilifikia makubaliano ya kusimamisha mapigano Aprili 8 baada ya siku 40 za mapigano. Kufuatia usitishaji huo wa vita, wajumbe wa Iran na Marekani walifanya mazungumzo ya amani ya raundi moja mjini Islamabad Aprili 11 na 12, ambayo hayakufanikiwa kuleta makubaliano.

Katika kipindi cha wiki zilizopita, pande hizo mbili zimeripotiwa kubadilishana mipango kadhaa iliyopendekezwa inayoelezea masharti ya kukomesha mgogoro huo kupitia upatanishi wa Pakistan.

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha