Baraza la Usalama la UN laongeza muda wa vikwazo dhidi ya makundi yenye silaha ya Jamhuri ya Afrika ya Kati

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 30, 2026

UMOJA WA MATAIFA - Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha azimio la kuongeza muda wa vikwazo kwa mwaka mmoja dhidi ya makundi yenye silaha yanayofanya shughuli katika Jamhuri ya Afrika ya Kati (CAR) pamoja na watu wengine wanaoharibu amani nchini humo, vikwazo hivyo vitaendelea hadi Tarehe 31 Julai, 2027.

Azimio hilo No.2827, lililopitishwa kwa kauli moja na baraza hilo la wajumbe 15, pia limeongeza muda wa jukumu la jopo la wataalamu linalosaidia utekelezaji wa vikwazo hivyo hadi Agosti 31, 2027.

Baraza hilo la Usalama mwaka 2024 liliondoa marufuku ya usafirishaji wa silaha kwa serikali ya CAR, lakini likidumisha vikwazo vya silaha kwa makundi yenye silaha na watu wanaohusika nayo wanaofanya shughuli katika CAR, vilevile hatua mahsusi za kuzuia mali na kupiga marufuku ya usafiri dhidi ya makundi na watu binafsi waliobainishwa na Kamati ya Vikwazo.

(Wahariri wa tovuti:Liu Mengxue,Zhao Jian)

Picha