Lugha Nyingine
Hamas yahimiza shinikizo kwa Israel kuidhinisha mpango wa awamu ya pili ya makubaliano ya kusimamisha mapigano Gaza

Wapalestina wakihudhuria mazishi ya halaiki ya waathiriwa 112 katika Mji wa Gaza, Agosti 4, 2026. (Picha na Rizek Abdeljawad/Xinhua)
GAZA – Hamas imetoa wito kwa wapatanishi na wahakikishaji kuishinikiza Israel kuidhinisha mpango wa awamu ya pili ya makubaliano ya kusimamisha mapigano Gaza.
Wito huo umetolewa jana Jumapili katika taarifa iliyotolewa kufuatia mkutano wa jijini Cairo kati ya ujumbe wa Hamas, ambao uliongozwa na Khalil al-Hayya, mkuu wa ofisi ya siasa ya Hamas, na wawakilishi wa wapatanishi na wadhamini wa makubaliano ya kusimamisha mapigano.
Ujumbe huo umehimiza wapatanishi na "Bodi ya Amani" inayoongozwa na Marekani kuishinikiza Israel kutekeleza ahadi zake zote chini ya awamu ya kwanza ya makubaliano, kusimamisha mauaji na uvamizi wa ardhini, na kuidhinisha mpango wa awamu ya pili ya makubaliano, taarifa hiyo inasomeka.
Hamas pia imesema imekubali mpango huo, ikirejelea lengo lake la kupata usimamishaji mapigano wa kudumu, kujiondoa kikamilifu kwa Israel kutoka Gaza, misaada endelevu ya kibinadamu, na kuanza kazi kwa Kamati ya Kitaifa ya Utawala wa Gaza, imesema.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema mapema mwezi huu kwamba Israel imekataa mpango huo unaoungwa mkono na Marekani na haitaondoa vikosi vyake kutoka Gaza hadi Hamas itakaponyang'anywa silaha kikamilifu.
"Bodi ya Amani" ilichapisha mpango wa pointi 15 Julai 31 kwa ajili ya kutekeleza awamu inayofuata ya makubaliano ya Gaza. Unajumuisha kukomeshwa kwa operesheni za kijeshi, kuhamishia utawala wa kiraia kwa Kamati ya Kitaifa ya Utawala wa Gaza, kukabidhiwa kwa silaha nzito, ghala za silaha, vituo vya uzalishaji na mahandaki ya kijeshi, pamoja na mipangilio kwa ajili ya kujiondoa kwa Israeli.
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma



