人民网首页

Hadithi

Mpiga picha akibeba mkoba wa Michezo ya Olimpiki ya Beijing 2008 katika kituo cha vyombo vya habari cha Michezo ya Olimpiki ya Beijing 2022

Huku zikiwa zimebaki siku chini ya 30 kabla ya kufunguliwa kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing, baadhi ya waandishi wa habari wameonekana katika kituo cha vyombo vya habari cha michezo hiyo wakibeba mikoba ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya joto ya Beijing 2008 ambayo waandishi wa habari walipewa bure. Mpiga picha wa Iran alisema anabeba mkoba huo kila akipiga picha kwenye mashindano ya michezo.

Januari 12, Mwaka 2022, Mwenyeji wa Beijing Zhang Wenquan akionesha saini za mabingwa wa China kwenye Michezo ya Olimpiki ya Beijing ya Mwaka 2008 huko Beijing.

“Makumbusho madogo ya Michezo ya Olimpiki” katika kichochoro cha Bejing

Zhang amekusanya na kuhifadhii vitu zaidi ya 5000 kuhusu Michezo ya Olimpiki, vikiwemo bendera za Michezo ya Olimpiki, vitu vya baraka, myenge n.k.

Wang Yang akichunguza soli ya viatu yenye makali kwa ajili ya kuteleza kwenye barafu. (Picha/Chinanews.com)

Aliyekuwa Mchezaji Aanzisha Kampuni kutengeneza Viatu vya Kuteleza kwenye Barafu kwa wa Wanariadha wa kulipwa wa China

“Sikuweza kushiriki kwenye Michezo ya Olimipiki. Ninatumai kwamba wachezaji wa China wanaovaa viatu vya kuteleza kwenye barafu ninavyotengeneza wataleta medali za dhahabu nyumbani” anasema Wang Yang, mtengenezaji wa viatu vya kuteleza kwenye barafu, ambaye aliwahi kuwa mchezaji wa mbio za kuteleza kwa kasi katika mduara mfupi kwenye barafu.

Mshiriki mwenye matumaini ya kushiriki Michezo ya Olimpiki, Zahra Sulghani akiteleza kwa kasi kwenye theluji wakati wa shindano la kufuzu kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing 2022 kwenye Uwanja wa Kuteleza kwenye theluji wa Hoteli ya Darbandsar huko Iran siku ya Jumapili ya wiki iliyopita (XINHUA)

Wanamichezo wa kuteleza kwenye theluji wa Iran wajawa na matumaini ya Olimpiki

TEHERAN- Huku Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing ikikaribia, wanamichezo wa Iran wa kuteleza kwa kasi kwenye milima ya theluji ya Alpine wanawania nafasi ya kushindana kwenye jukwaa kubwa zaidi la michezo mjini Beijing. "Natumai nitaweza kufuzu kwa Michezo ya Olimpiki ya Majira ya baridi ya Beijing na ningependa sana kwenda China," anasema Fatemeh Kia Shemshaki mwenye umri wa miaka 17, mwanamichezo wa alpine ambaye anashiriki katika mashindano yanayoendelea ya kufuzu kwa Michezo ya Olimpiki huko Iran kwenye Uwanja wa Kuteleza kwenye theluji wa Hoteli ya Darbandsar.

Iliyopita1 2