Kaburi la Mfalme Wen wa Enzi ya Han ya China lagunduliwa Shaanxi

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Desemba 15, 2021
Kaburi la Mfalme Wen wa Enzi ya Han ya China lagunduliwa Shaanxi

Jumanne ya wiki hii, Taasisi ya utafiti wa mabaki ya kale ya Shaanxi imesema, kaburi kubwa la Jiangcun lililoko kwenye mwisho wa Magharibi mwa Bailuyuan, katika kitongoji cha Mashariki mwa Mji wa Xi'an, Shaanxi, na mabaki mengine ya kale yanayozunguka eneo hilo yanaundwa kuwa eneo kamili la kaburi lenye muonekano unaofanana na kaburi la Mfalme Wen wa Enzi ya Han (K.K. 202-B.K.220). Mpangilio wa muundo kwa ujumla ni sawa na kuna dalili za maendeleo dhahiri na mwelekeo wa mabadiliko. Taasisi hiyo imelinganisha eneo hilo na kumbukumbu za nyaraka za historia na kupata hitimisho kuwa, eneo hilo ndilo la kaburi la Mfalme Wen wa Enzi ya Han.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha