Mnara wa Nembo ya Maduara Matano ya Olimpiki Wakaribisha Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Januari 12, 2022
Mnara wa Nembo ya Maduara Matano ya Olimpiki Wakaribisha Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi
(Picha zinatoka tovuti ya Shirika la Habari la China Xinhua.)

Hivi karibuni, kazi ya kufunga “Mnara wa Haituo” wa Nembo ya Maduara Matano ya Olimpiki imekamilika. Mnara huo uko kwenye eneo la michezo la Yanqing la Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing, na sasa ujenzi wa mradi huo umekaribia kukamilika. Juu ya mnara huo, kumewekwa nembo ya Maduara Matano ya Olimpiki. Jumla ya taa nyeupe zaidi ya elfu 70 zimefungwa kwenye nembo hiyo na mapambo yenye umbo la riboni yameongezwa kwenye mnara.

Habari husika zimesema, kazi ya kufunga “Mnara wa Haituo” unatazamiwa kukamilika kabla ya mwisho wa Januari, 2022, ambapo taa zake zitawashwa na kuwa moja ya mandhari ya kipekee ya Michezo ya Olimpiki ya Majira ya Baridi ya Beijing.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha