Rais wa China Xi Jinping akagua Mji wa Urumqi katika Xinjiang ya China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 15, 2022
Rais wa China Xi Jinping akagua Mji wa Urumqi katika Xinjiang ya China
Rais Xi Jinping wa China, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Kijeshi ya China, akitembelea Chuo Kikuu cha Xinjiang huko Urumqi, Mji Mkuu wa Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Uygur, Kaskazini Magharibi mwa China, Julai 12, 2022. (Xinhua/ Li Xueren)

URUMQI - Rais Xi Jinping wa China, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China alifanya ziara ya kukagua chuo kikuu, eneo la bandari ya kimataifa ya nchi kavu, jumuiya ya makazi na jumba la makumbusho huko Urumqi, Xinjiang, China kuanzia Jumanne alasiri hadi Jumatano asubuhi.

Xi alitembelea Chuo Kikuu cha Xinjiang, Eneo la Bandari ya Kimataifa ya Nchi kavu ya Urumqi, jumuiya ya Guyuanxiang iliyopo Wilaya ya Tianshan na Makumbusho ya Mkoa unaojiendesha wa Xinjiang Uygur.

Xi alifahamishwa kuhusu kazi ya kukuza vipaji, kuratibu kazi za kukabiliana na maambukizi ya virusi vya korona na maendeleo ya kiuchumi na kijamii, kuhimiza mshikamano na maendeleo ya makabila mbalimbali na kuongeza uelewa kuhusu jumuiya yenye mustakabali wa pamoja ya Taifa la China.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha