China yajiandaa kurusha chombo cha anga ya juu cha Shenzhou-15 (3)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Novemba 22, 2022
China yajiandaa kurusha chombo cha anga ya juu cha Shenzhou-15
Chombo cha anga ya juu cha Shenzhou-15 na roketi ya kubeba ya Long March-2F vikiwa tayari kuhamishiwa kwa pamoja katika eneo la Kituo cha Kurusha Satelaiti cha Jiuquan, Kaskazini-Magharibi mwa China, Novemba 21, 2022. (Picha na Wang Jiangbo/Xinhua)

JIUQUAN - Chombo cha anga ya juu cha Shenzhou-15 na roketi ya kubeba ya Long March-2F kwa pamoja siku ya Jumatatu vimehamishiwa katika eneo la Kituo cha Kurusha Satelaiti cha Jiuquan, Kaskazini-Magharibi mwa China, Shirika la Anga ya Juu la China (CMSA) limesema.

Miundombinu na vifaa kwenye eneo la urushaji viko katika hali nzuri, na ukaguzi wa ufanisi wa kabla ya urushaji na majaribio ya pamoja yatafanywa kama ilivyopangwa, imesema CMSA.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha