Afghanistan yapokea magari mapya ya kubebea wagonjwa 125 (2)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Novemba 25, 2022
Afghanistan yapokea magari mapya ya kubebea wagonjwa 125
Picha hii iliyopigwa Tarehe 23 Novemba 2022 ikionyesha magari ya kubebea wagonjwa yaliyopokelewa Kabul, Afghanistan. (Picha na Sabawoon/Xinhua)

KABUL - Wizara ya Afya ya Umma ya Afghanistan siku ya Jumatano imepokea magari mapya ya kubebea wagonjwa 125 kati ya 180 yaliyotolewa kupitia mkataba na Uzbekistan, Sharafat Zaman, msemaji wa wizara hiyo, amesema Alhamisi.

"Magari ya kubeba wagonjwa, yenye thamani ya dola za Kimarekani 6,051,000, yamekabidhiwa kwa Wizara ya Afya ya Umma ili kuboresha huduma za afya ya umma katika mji mkuu na majimbo ya nchi," Zaman ameliambia Shirika la Habari la China, Xinhua.

Serikali ya uangalizi ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban imeapa kuboresha huduma za umma ikiwemo afya kote nchini humo, wakati huu ambapo watu wanakosa huduma za afya za kutosha katika maeneo mengi ya nchi hiyo iliyokumbwa na vita.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha