Misemo iliyonukuliwa na Rais wa China Xi Jinping (3)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 07, 2023

Mwaka huu unatimiza miaka 100 ya kuzaliwa kwa Nelson Mandela. Acha ninukuu moja ya misemo yake maarufu, "Baada ya kupanda kilima kikubwa, mtu hutambua tu kwamba kuna vilima vingi zaidi vya kupanda." Hakika, historia ya ushirikiano wa BRICS ni safari ya nchi zetu tano kupanda kilima kikubwa ili kufikia urefu mpya. Ninasadiki kwamba pale nchi zetu tano zitakaposonga mbele pamoja, tutapanda vilele vipya, kufikia urefu mpya, na kutoa mchango mkubwa zaidi kwa amani na maendeleo ya binadamu.

—— Hotuba ya Rais wa China Xi Jinping katika Baraza la Biashara la BRICS nchini Afrika Kusini Julai 25, 2018

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha