Xi Jinping asisitiza maendeleo yasiyochafua mazingira wakati wa ukaguzi wa Mongolia ya Ndani

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Juni 09, 2023
Xi Jinping asisitiza maendeleo yasiyochafua mazingira wakati wa ukaguzi wa Mongolia ya Ndani
Kuanzia tarehe 7 hadi 8, mwezi Juni, Rais wa China Xi Jinping alifanya ukaguzi katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani. Picha ikionesha asubuhi ya tarehe 8, Rais Xi Jinping alisikiliza ripoti ya kazi ilitolewa na kamati ya Chama na serikali ya Eneo linalojiendesha la Mongolia ya Ndani, na akitoa hotuba muhimu huko Hohhot. (Picha ilipigwa na Ju Peng/Xinhua)

Rais wa China Xi Jinping, ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Kijeshi ya China (CMC) hivi karibuni alipofanya ukaguzi katika Mongolia ya Ndani alisisitiza kuwa, ni lazima kushikilia nafasi ya kimkakati ya Mongolia ya Ndani iliyopangwa na Kamati Kuu ya Chama, kutekeleza kikamilifu, kwa usahihi na kwa pande zote wazo jipya la maendeleo, kuhimiza bila kulegalega kazi kuu ya kwanza ya kujipatia maendeleo ya hali ya juu, kuweka mkazo katika kazi mbili za maendeleo na usalama, kutoa kipaumbele kwa ulinzi wa mazingira ya asili na kuelekea kupata maendeleo yasiyochafua mazingira, kushiriki na kuhudumia kwa hamasa ujenzi wa muundo mpya wa maendeleo, na kufanya juhudi za kuandika sura mpya ya Mongolia ya Ndani ya maendeleo ya kisasa yenye umaalumu wa China.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha