Idadi ya vifo vya Wapalestina katika mashambulizi ya Israel yafikia 1,417 (4)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Oktoba 13, 2023
Idadi ya vifo vya Wapalestina katika mashambulizi ya Israel yafikia 1,417
Watu wakikagua majengo yaliyobomolewa na mashambulizi ya anga ya Israel katika Mji wa Rafah ulioko Kusini mwa Ukanda wa Gaza, Oktoba 12, 2023. (Picha na Khaled Omar/Xinhua)

GAZA - Idadi ya vifo vya Wapalestina katika mashambulizi yanayoendelea ya Israel huko Gaza imefikia 1,417, huku wengine 6,268 wakijeruhiwa, kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Afya ya Gaza.

Israel siku ya Alhamisi iliendelea na mashambulizi yake ya anga katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza.

Mashambulizi hayo ya anga yanatekelezwa kwa kujibu mashambulizi makubwa ya kushtukiza yaliyoanzishwa na Kundi la Hamas siku ya Jumamosi.

Shirika la Utangazaji la Israel la Kan limesema kuwa idadi ya vifo nchini Israel imeongezeka na kufikia zaidi ya 1,300. 

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha