Rais Xi Jinping akagua Mji wa Nanning katika Mkoa wa Guangxi, Kusini mwa China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Desemba 15, 2023
Rais Xi Jinping akagua Mji wa Nanning katika Mkoa wa Guangxi, Kusini mwa China
Xi Jinping, Rais wa China ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), akizungumza na wakazi alipokuwa akikagua sehemu ya makazi ya Panlong ya Eneo la Liangqing la Mji wa Nanning, Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wazhuang wa Guangxi, Kusini mwa China, Desemba 14, 2023. (Xinhua/Yan Yan)

NANNING - Xi Jinping, Rais wa China ambaye pia ni Katibu Mkuu wa Kamati Kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC), amekagua mji wa Nanning, ambao ni mji mkuu wa Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wazhuang wa Guangxi, Kusini mwa China siku ya Alhamisi asubuhi. Katika ukaguzi huo, ametembelea Kampuni ya China-ASEAN Information Harbor na sehemu ya makazi ya Panlong katika Wilaya ya Liangqing, na kufanya ufahamu wa kivitendo kuhusu ushirikiano wa kiuchumi na kibiashara kati ya China na Jumuiya ya Nchi za Asia Kusini Mashariki (ASEAN), maendeleo na matumizi ya taarifa, uboreshaji wa mfumo wa utawala wa sehemu za makazi za mijini na kuimarisha umoja wa kikabila.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha