Umoja wa Mataifa, Ubalozi wa China nchini Kenya zaandaa tamasha la Sikukuu ya Mwaka Mpya wa jadi wa China

(CRI Online) Februari 01, 2024
Umoja wa Mataifa, Ubalozi wa China nchini Kenya zaandaa tamasha la Sikukuu ya Mwaka Mpya wa jadi wa China
(Picha na Huang Weixin/People's Daily Online)

Umoja wa Mataifa na Ubalozi wa China nchini Kenya na Shirika Kuu la Utangazaji la China (CMG) zimeandaa tamasha la kukaribisha Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China mjini Nairobi.

Kwenye tamasha hilo liliohudhuriwa na maofisa waandamizi wa Umoja wa Mataifa, wanadiplomasia na wasomi, Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa mjini Nairobi Bibi Zainab Hawa Bangura, amesema kwa mara ya kwanza Sikukuu ya Mwaka Mpya wa Jadi wa China imetambuliwa na kuingizwa kwenye kalenda ya sikukuu ya Umoja wa Mataifa. Ofisa huyo ameeleza matumaini yake kuwa sikukuu hiyo italeta amani, furaha, afya njema na ustawi kwa binadamu.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha