Njia ya kutazama mandhari ya treni ya Maglev yashamirisha utalii katika mji wa kale wa Fenghuang, China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Februari 04, 2024
Njia ya kutazama mandhari ya treni ya Maglev yashamirisha utalii katika mji wa kale wa Fenghuang, China
Picha iliyopigwa Februari 2, 2024 ikionyesha stesheni ya Fenghuang ya treni ya Maglev ya kutazamia mandhari kwenye Mji wa kale wa Fenghuang katika mji unaojiendesha wa Makabila ya Watujia na Wamiao wa Xiangxi, Mkoa wa Hunan, Katikati mwa China. (Xinhua/Chen Zhenhai)

FENGHUANG - Njia ya kutazama mandhari ya treni ya Maglev ya Fenghuang ilifunguliwa rasmi Julai 30, 2022. Njia hiyo inaanzia stesheni ya mji wa kale cha Fenghuang, ikiwa na urefu wa kilomita 9.121, ikiunganisha maeneo mbalimbali ya vivutio vya utalii katika mji wa kale wa Fenghuang katika mji unaojiendesha wa Makabila ya Watujia na Wamiao wa Xiangxi, Mkoa wa Hunan, Katikati mwa China. Abiria wanaweza kufurahia mandhari nzuri nje ya madirisha ya treni wakiwa njiani.

Wakati wa Mwaka Mpya wa Jadi wa China, treni hiyo ya Maglev ya Fenghuang inatarajiwa kusafirisha abiria zaidi ya 10,000 kila siku.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha