Watawa 12 wapata shahada yenye hadhi sawa na uzamivu katika Ubuddha wa Tibet, China

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Februari 29, 2024
Watawa 12 wapata shahada yenye hadhi sawa na uzamivu katika Ubuddha wa Tibet, China
Watawa wakishiriki kwenye shughuli ya mdahalo wa shahada ya Geshe Lharampa katika Hekalu la Jokhang huko Lhasa, mji mkuu wa Mkoa wa Xizang, Kusini Magharibi mwa China, Februari 28, 2024. (Xinhua/Tenzing Nima Qadhup)

LHASA - Watawa kumi na wawili wamepata shahada yenye hadhi sawa na ya uzamivu ya Geshe Lharampa ambayo ni shahada ya juu zaidi ya mafunzo ya nje ya mazingira yao ya kawaida katika elimu ya kisasa ya shule ya Gelug ya Ubuddha wa Tibet, kufuatia mdahalo wa sutra uliofanyika siku ya Jumatano katika Mkoa wa Xizang, Kusini Magharibi mwa China.

Wakitokea Mkoa huo wa Xizang na Mkoa wa Yunnan wa Kusini-Magharibi mwa China, watawa hao 12 walishiriki kwenye mdahalo na hafla ya kutoa shahada zao iliyofanyika kwenye Hekalu la Jokhang huko Lhasa, mji mkuu wa mkoa huo.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha