Mji wa Fuzhou waendeleza ufugaji samaki wa dhahabu

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Machi 15, 2024
Mji wa Fuzhou waendeleza ufugaji samaki wa dhahabu
Maofisa wa forodha wakikagua samaki wa dhahabu watakaosafirishwa nje ya nchi mjini Fuzhou, Mkoa wa Fujian, Kusini Mashariki mwa China, Machi 14, 2024. (Xinhua/Wei Peiquan)

Katika miaka ya hivi karibuni, mji wa Fuzhou katika Mkoa wa Fujian, Kusini Mashariki mwa China wenye historia ya miaka zaidi ya 400 ya kuzaliana na kufuga samaki wa dhahabu, umebuni mbinu ya uzalianaji na ufugaji wa samaki hao ambayo ni endelevu, ya kitaalamu na kuzingatia ikolojia. Mwaka 2022, eneo la kuzaliana na kufuga samaki hao la Fuzhou lilifikia ukubwa wa karibu mu 2,500 (kama hekta 166.7), na lina kampuni zaidi ya 100 zinazojihusisha na kazi hiyo ambazo uzalishaji wa kila mwaka wa samaki hao zaidi ya milioni 15 na mapato yatakanayo na uzalishaji huo yamefikia yuan bilioni 1 (kama dola za Kimarekani milioni 139). 

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha