Rais Xi Jinping afanya ziara ya ukaguzi mjini Chongqing

(CRI Online) April 24, 2024
Rais Xi Jinping afanya ziara ya ukaguzi mjini Chongqing
(Picha inatoka Xinhua.)

Rais Xi Jinping wa China amefanya ziara ya ukaguzi mjini Chongqing kuanzia tarehe 22 hadi 23 mwezi huu ambapo katika ziara hiyo, ametembelea Kituo cha Usafirishaji Bidhaa cha Kimataifa cha Chongqing, jumuiya ya makazi ya mtaa wa Xiejiawan wilayani Jiulongpo, na Kituo cha Uendeshaji na Usimamizi wa Mji wa Kidijitali cha Chongqing.

Amefahamishwa juu ya hali ya mji huo katika kuharakisha ujenzi wa Ushoroba Mpya wa Kimataifa wa Kuunganisha Bahari na Nchi kavu katika sehemu ya magharibi ya China, kufanya maboresho kwa mji na maisha ya wakazi, na kuinua kiwango cha usimamizi wa kisasa wa mji.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha