Maonyesho ya Kimataifa ya Magari ya Beijing 2024 yashuhudia mwelekeo wa maendeleo ya viwanda vya magari duniani

(Tovuti ya Gazeti la Umma) April 26, 2024
Maonyesho ya Kimataifa ya Magari ya Beijing 2024 yashuhudia mwelekeo wa maendeleo ya viwanda vya magari duniani
Wadau wa tasnia wakifuatilia kwa makini Maonyesho ya Kimataifa ya Magari ya Beijing 2024. (Picha na Jiao Lei, People's Daily Online)

Maonyesho ya 18 ya Kimataifa ya Magari ya Beijing 2024 yakiwa na kaulimbiu ya "Zama Mpya, Magari Mapya" yanafanyika kuanzia Aprili 25 hadi Mei 4, 2024 kwenye Ukumbi wa Shunyi na Ukumbi wa Chaoyang wa Kituo cha Maonyesho cha Kimataifa cha China mjini Beijing. Maonyesho hayo ya Magari ya Beijing yamevutia chapa nyingi za magari za ndani na nje ya China kuonesha bidhaa zao mpya. Jumla ya magari 117 yanayooneshwa kwa mara ya kwanza duniani, ikijumuisha magari 30 yanayooneshwa kwa mara ya kwanza duniani kutoka kampuni za kimataifa, magari mapya yaliyobuniwa 41, na magari ya aina 278 yanayotumia nishati mpya yanaonyeshwa.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Renato Lu)

Picha