Mkutano wa Kilele wa 6 wa Vyombo vya Habari Duniani wafunguliwa Urumqi, China (4)

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Oktoba 15, 2024
Mkutano wa Kilele wa 6 wa Vyombo vya Habari Duniani wafunguliwa Urumqi, China
Mtu akijaribu kupiga dutar, ala ya nyuzi, kwenye ukumbi wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Kilele wa 6 wa Vyombo vya Habari Duniani huko Urumqi, mji mkuu wa Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wauygur wa Xinjiang, Kaskazini-Magharibi mwa China, Oktoba 14, 2024. (Xinhua/Chen Yehua)

URUMQI - Mkutano wa Kilele wa 6 wa Vyombo vya Habari Duniani wenye kaulimbiu ya "Akili Bandia na Mageuzi ya Vyombo vya Habari," umefunguliwa jana Jumatatu asubuhi huko Urumqi, mji mkuu wa Mkoa unaojiendesha wa Kabila la Wauygur wa Xinjiang, Kaskazini-Magharibi mwa China ukikutanisha washiriki zaidi ya 500 kutoka nchi na maeneo 106, wakiwemo wawakilishi 208 wa vyombo vikuu vya habari, mashirika ya kiserikali na mashirika ya kimataifa.

Mkutano huo umeandaliwa kwa pamoja na Shirika la Habari la China, Xinhua na serikali ya Mkoa wa Xinjiang.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha