Hafla ya Kukaribisha Panda wa China yafanyika katika Bustani ya Wanyama ya Adelaide, Australia

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Januari 22, 2025
Hafla ya Kukaribisha Panda wa China yafanyika katika Bustani ya Wanyama ya Adelaide, Australia
Waziri Mkuu wa Jimbo la Australia Kusini, nchini Australia Peter Bryden Malinauskas, akitoa hotuba katika hafla ya kukaribisha panda iliyofanyika kwenye Bustani ya Wanyama ya Adelaide, Januari 21. (Picha na Zhang Jianhua/ Xinhua)

Serikali ya Jimbo la Australia Kusini nchini Australia imefanya hafla ya kukaribisha panda wawili wapya wa China katika Bustani ya Wanyama ya Adelaide Januari 21. Panda dume“Xing Qiu”na panda jike“Yi Lan” walifika Adelaide kwa ndege maalum Desemba15, 2024, wakianza raundi mpya ya ushirikiano wa utafiti kati ya China na Australia kuhusu uhifadhi wa panda. Kwa mujibu wa makubaliano, panda hao wataishi Australia kwa kipindi cha miaka 10.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha