Upinzani nchini Sudan Kusini wadai kushikilia maeneo ya mpakani

(CRI Online) Mei 12, 2025

Chama cha upinzani cha SPLM-IO cha nchini Sudan Kusini kinachoongozwa na Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi hiyo, Riek Machar, kimedai kuwa kimedhibiti tena miji kadhaa karibu na mipaka ya Sudan Kusini na Uganda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Msemaji wa SPLM-IO Lam Paul Gabriel amesema katika taarifa iliyotolewa Juba, juzi Jumamosi, kwamba wamedhibiti maeneo ya Kendila, Panyume, Mongoya na Lujulo katika Jimbo la Ikweta ya Kati siku ya Alhamis baada ya mapambano kati yake na Jeshi la Ulinzi la Sudan Kusini na Vikosi vya Usalama wa Taifa.

Mapigano kati ya pande hizo mbili yameongezeka tangu tarehe 26 Machi mwaka huu katika maeneo mbalimbali ya Sudan Kusini, hususan katika majimbo ya Upper Nile, Unity na Ikweta ya Kati.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha