Watu 62 wafariki kutokana na mafuriko mashariki mwa DRC

(CRI Online) Mei 12, 2025

Watu 62 wamefariki kufuatia mafuriko yaliyokumba eneo la Fizi katika Jimbo la Kivu Kusini, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) usiku wa kuamkia Ijumaa hadi Jumamosi.

Mpaka sasa, mvua kubwa imesababisha mafuriko katika eneo la Kasaba, na kubomoa nyumba 150, kujeruhi watu 30, na wengine kadhaa bado hawajulikani walipo.

Serikali ya jimbo hilo imeeleza wasiwasi mkubwa juu ya kuongezeka kwa hatari ya magonjwa yatokanayo na maji, yakiwemo ya mfumo wa upumuaji na utapiamlo, kutokana na mvua hizo.

Majimbo mengine mengi likiwemo la Tanganyika pia yanakabiliwa na mafuriko yanayotokea mara kwa mara kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha