

Lugha Nyingine
China yaingia zama ya 5G-A
China inaharakisha ufungaji wa mitandao ya 5G- ya hali ya juu (5G-A) katika miji mbalimbali, ikiwemo Beijing na Shanghai, ikiashiria mafanikio makubwa katika kasi na muunganisho wakati ambapo waendeshaji wa huduma za mawasiliano ya simu wakiboresha ufikaji huduma katika njia za sabwei, maeneo ya kibiashara na vijijini.
5G-A pia inaitwa jina la 5.5G na baadhi ya watengenezaji na inawakilisha uboreshaji zaidi wa 5G na hatua kuelekea muunganisho wa 6G. Inatoa maboresho makubwa katika uwezo, kasi, muda wa kuunganisha, na nafasi na ni hadi mara 10 zaidi ya 5G katika suala la kasi ya intaneti.
Kwa mujibu wa wafanyakazi kutoka kampuni kuu zinazoendesha mawasiliano ya simu nchini China, modeli nyingi za simu janja za kawaida kwenye soko tayari zinalandana na mitandao ya 5G-A, ikiruhusu watumiaji kufurahia kasi ya haraka bila kutozwa gharama za ziada.
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
Shaolin Kungfu, chombo muhimu cha mawasiliano ya Utamaduni wa China na ulimwengu wa nje
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma