

Lugha Nyingine
Kenya kuongeza mauzo ya chai yake nchini China
Kenya inalenga kuongeza mauzo ya chai yake nchini China kwa zaidi ya mara nne katika miaka sita ijayo.
Waziri wa Kilimo na Maendeleo ya Mifugo wa Kenya, Mutahi Kagwe amesema, lengo ni kuongeza mauzo hayo ya chai ya Kenya nchini China kutoka kilogramu milioni 12.42 za mwaka 2024 hadi kilogramu milioni 50 itakapofika mwaka 2030.
Waziri Kagwe amesema hayo katika taarifa iliyotolewa jijini Nairobi, baada ya kukutana na Zhang Chaobin, mwenyekiti wa Kampuni ya Chai ya Benny ya mkoani Fuzhou, China.
Kagwe amesema mkutano huo ni sehemu ya juhudi za kuongeza uwepo wa Kenya katika soko la chai la China, akiongeza kuwa, mawasiliano hayo ya ngazi ya juu yanaonyesha mkakati wa Kenya wa kuboresha mauzo yake ya chai ya kipekee nchini China.
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
Shaolin Kungfu, chombo muhimu cha mawasiliano ya Utamaduni wa China na ulimwengu wa nje
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma