Jukwaa la Wakurugenzi Afrika lafunguliwa nchini Cote d’Ivoire

(CRI Online) Mei 14, 2025

Mkutano wa 12 wa Jukwaa la Wakurugenzi Afrika umeanza Jumatatu wiki hii katika mji mkuu wa Cote d’Ivoire, Abidjan, chini ya kaulimbiu ya “Je Inawezekana Makubaliano Mapya kati ya Serikali na Sekta Binafsi Kulipatia Bara Mkono wa Kushinda?”

Karibu wafanyabiashara 2,500 na maofisa wa umma kutoka nchi zaidi ya 75 wanashiriki katika mkutano huo, ambao unalenga kuanzisha makubaliano mapya kati ya nchi za Afrika na wafanyabiashara ili kuongeza kasi ya mageuzi ya kiuchumi katika bara hilo.

Akizungumza katika ufunguzi wa mkutano huo, Rais wa Cote d’Ivoire Alassane Ouattara ametoa wito kwa watunga sera barani Afrika kufikiria upya mifumo ya uratibu kati ya sekta binafsi na sekta ya umma.

Mkutano huo wa siku mbili ulilenga katika juhudi za kuboresha uongozi, kuboresha sera za umma, na kuongeza kasi ya utekelezaji wa Eneo la Biashara Huria la Afrika.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha