Wataalam wakutana Kenya kujadili kuendeleza hidrojeni ya kijani katika Afrika Mashariki

(CRI Online) Mei 15, 2025

Watunga sera, wataalamu wa nishati, na wenzi wa maendeleo wamekutana jana Nairobi, Kenya, kujadili njia za kuendeleza matumizi ya hidrojeni ya kijani kuwa kichocheo cha nishati endelevu na mageuzi ya kiuchumi katika eneo la Afrika Mashariki.

Mkutano huo wa siku mbili wa Hidrojeni ya Kijani wa Afrika Mashariki umeshirikisha zaidi ya washiriki 200, na kutengeneza njia ya kikanda kwa ajili ya kujenga uchumi endelevu wa hidrojeni ya kijani.

Waziri wa Nishati na Mafuta nchini Kenya James Opiyo Wandayi, amesema Kenya inafanya juhudi kutumia raslimali zake za nishati mbadala kutengeneza hidrojeni kwa matumizi katika sekta ya kemikali, na kupunguza utoaji wa kaboni katika sekta ya usafiri.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha