

Lugha Nyingine
Usafirishaji wa mizigo kwa treni ya SGR ya Kenya waongezeka kwa asilimia 40 katika robo ya kwanza ya mwaka
Shirika la Reli la Kenya (KRC) limesema katika ripoti iliyotolewa jana Jumatano kuwa, mahitaji ya huduma ya usafirishaji wa mizigo ya Reli ya SGR nchini Kenya yameongezeka kwa asilimia 40 katika robo ya kwanza ya mwaka huu.
Ripoti hiyo pia imesema, reli ya SGR ilisafirisha tani milioni 1.82 za mizigo katika kipindi cha miezi mitatu, kutoka tani milioni 1.3 katika kipindi kama hicho mwaka jana.
Aidha, mapato kutokana na huduma ya usafiri wa abiria yalipanda hadi shilingi bilioni 3.82 za Kenya (sawa na dola za kimarekani milioni 29.5) katika kipindi hicho, kutoka dola milioni 25 mwaka jana.
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
Shaolin Kungfu, chombo muhimu cha mawasiliano ya Utamaduni wa China na ulimwengu wa nje
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma