

Lugha Nyingine
Kenya yazindua jukwaa la wingu kuboresha usambazaji wa chanjo
Wizara ya Afya nchini Kenya imezindua jukwaa la wingu ili kuhakikisha kuwa chanjo zinawasilishwa katika maeneo ya nchi hiyo bila ya usumbufu.
Waziri wa Wizara hiyo Aden Duale amesema, Mlango wa Kitaifa wa Kielektroniki wa Chanjo na Kinga utaanzisha hazina ya wakati halisi ya usimamizi wa takwimu za chanjo na kinga. Amesema jukwaa hilo la kidijitali litaboresha utoaji maamuzi na kuongeza uwazi, ufuatiliaji, uwajibikaji, na ufanisi katika huduma ya usambazaji wa chanjo nchini humo.
Amesema mlango huo unalenga kuimarisha miundombinu ya kinga nchini Kenya huku ukilinda afya ya watoto na watu wa makundi mengine yaliyo hatarini.
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
Shaolin Kungfu, chombo muhimu cha mawasiliano ya Utamaduni wa China na ulimwengu wa nje
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma