Rais wa zamani wa Mauritania ahukumiwa kifungo cha miaka 15 jela kwa makosa ya ufisadi

(CRI Online) Mei 16, 2025

Mahakama ya rufani nchini Mauritania jumanne wiki hii imemhukumu rais wa zamani wa nchi hiyo, Mohamed Ould Abdel Aziz, kifungo cha miaka 15 jela kutokana na ufisadi, matumizi mabaya ya madaraka, na utakatishaji fedha.

Awali, Aziz ambaye alikuwa rais wa Mauritania kuanzia Agosti 5, 2009 hadi Agosti Mosi, 2019, alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela katika hukumu ya kwanza.

Mwanasheria wake, Mohameden Ould Ichidou amesema, mteja wake anadhamiria kukata rufaa Mahakama Kuu, akidai kuwa, hukumu hiyo ya kufungwa jela miaka 15 imegubikwa na kile alichokiita matumizi mabaya ya madaraka.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha