Vyombo vya habari vya Ethiopia na China vyaahidi uhusiano wa karibu ili kuimarisha  mawasiliano ya kitamaduni

(CRI Online) Mei 16, 2025

Vyombo vya habari vya Ethiopia na China vimeeleza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kina ili kuboresha maelewano ya pamoja na kuimarisha mawasiliano ya kiutamaduni.

Kauli hiyo imetolewa wakati wa jukwaa la ngazi ya juu lililofanyika jumatano wiki hii mjini Addis Ababa, mji mkuu wa Ethiopia, chini ya kaulimbiu “Kuitazama China: Kuboresha Ushirikiano wa Vyombo vya Habari vya China na Ethiopia.”

Mkutano huo ulioandaliwa kwa pamoja na Idara kuu ya Radio na Televisheni ya China, Idara ya Huduma za Mawasiliano ya Serikali ya Ethiopia, na Ubalozi wa China nchini Ethiopia, ulikutanisha washiriki 200, wakiwemo maofisa waandamizi wa Ethiopia, wanadiplomasia wa China, wajumbe wa vyombo vya habari kutoka nchi zote mbili, wasomi, na watunga maudhui wa Afrika.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha