Kampuni ya kuunda magari ya China yazindua magari yake yanayotumia umeme katika soko la Ethiopia

(CRI Online) Mei 19, 2025

Kundi la Kampuni za GAC, ambalo ni muundaji magari kutoka mkoa wa Guangdong nchini China, limezindua aina mbili za magari yake yenye kutumia nishati ya umeme nchini Ethiopia, ikiwa ni mara ya kwanza kwa magari ya kundi hilo kuingia kwenye soko la Ethiopia.

Kundi hilo limezindua magari yake aina ya AION Y na ES9 katika hafla iliyofanyika Jumamosi mjini Addis Ababa.

Akiongea katika hafla hiyo, kamishna wa Kamisheni ya Uwekezaji ya Ethiopia, Zeleke Temesgen, amesema serikali ya nchi hiyo imechukua hatua madhubuti kuhamasisha matumizi ya magari yanayotumia umeme ili kuharakisha mpito wa nchi hiyo kuelekea usafiri wa kutumia umeme.

Kamishna huyo ametoa wito kwa kundi la GAC kujenga kiwanda cha kuunda magari nchini Ethiopia ili kutumia vizuri uwekezaji nafuu na fursa kubwa za soko nchini humo, na kuharakisha juhudi za Ethiopia kuelekea usafiri unaotumia nishati safi.

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha