

Lugha Nyingine
China yaendelea kuwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Afrika
Msaidizi wa Waziri wa Biashara wa China Tang Wenhong amesema, mwaka jana thamani ya biashara kati ya China na Afrika ilifikia dola bilioni 295.6 za Kimarekani, ongezeko la asilimia 4.8 ikilinganishwa na mwaka uliotangulia, na kuvunja rekodi kwa miaka 4 mfululizo.
Amesema, China imeendelea kuwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa Bara la Afrika kwa miaka 16 mfululizo.
Tang ametoa kauli hiyo kwenye mkutano na waandishi wa habari kuhusu Maonesho ya nne ya Uchumi na Biashara kati ya China na Afrika.
Maonyesho hayo yatafanyika kuanzia tarehe 12 hadi 15 mwezi ujao mjini Changsha, China, na hadi sasa zaidi ya watu elfu 12 kutoka nchi 44 za Afrika, mashirika 6 ya kimataifa, mikoa na miji 23 ya China, na zaidi ya mashirika 2,800 ya China na Afrika wamejiandikisha kuhudhuria maonesho hayo.
Miti ya jacaranda katika mchanuo wa maua yavutia watalii mjini Kunming, China
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
Maonyesho ya Kimataifa ya Baiskeli ya China 2025 yaanza Shanghai
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma