

Lugha Nyingine
Namibia yaidhinisha kujiunga na mfuko wa maendeleo ya kikanda wa SADC
Waziri wa teknolojia ya habari na mawasiliano wa Namibia Bibi Emma Theofelus ametoa taarifa akisema baraza la mawaziri la Namibia limeidhinisha kusaini makubaliano ya kujiunga na mfuko wa maendeleo ya kikanda (RDF) wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC).
Bibi Emma amesema kujiunga kwa Namibia kwenye mfuko huo kunatazamiwa kuboresha njia ya upatikanaji wa ufadhili wa maendeleo wa kikanda na kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi ndani ya SADC.
Ibara ya 26A ya mkataba wa SADC inatoa fursa ya kuanzishwa kwa mfuko huo kwa lengo la kukusanya rasilimali kutoka kwa nchi wanachama, washirika wa maendeleo, na sekta binafsi kusaidia maendeleo ya kikanda na kuimarisha ushirikiano wa kikanda.
Shughuli za kiutamaduni zafanyika kwenye Jukwaa la Russia na China mjini Khabarovsk, Russia
Miti ya jacaranda katika mchanuo wa maua yavutia watalii mjini Kunming, China
Upandaji mahindi waingia kipindi cha kilele katika Mkoa wa Mongolia ya Ndani, China
UNESCO latoa wito upya wa kuimarishwa ulinzi wa maeneo ya urithi ya Afrika
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma