

Lugha Nyingine
Tanzania yatoa wito wa kufanyika utafiti wenye tija kuleta mabadiliko katika sekta ya afya
Serikali ya Tanzania imehimiza watafiti na watunga sera kuwekeza katika utafiti wenye tija ili matokeo yake yatumike kutunga sera na mipango itakayoleta mageuzi katika sekta ya afya.
Wito huo umetolewa jana Jumatano na Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa, katika Kongamano la 13 la Kisayansi lililoandaliwa na Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi Shirikishi cha Muhimbili (MUHAS) linalofanyika kwenye kituo cha magonjwa ya moyo Kampasi ya Mloganzila.
Wito huo umeenda sambamba na wataalamu wa TEHAMA, afya na wasimamizi wa mifumo kuwekeza kwenye matumizi ya teknolojia katika kutoa huduma za afya ili kutambua na kuzuia magonjwa kupitia mifumo hiyo.
Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Daniel Mushi amesema uwekezaji mkubwa unaoendelea kufanywa na Serikali katika chuo hicho unachochewa na matokeo chanya ambayo MUHAS imekuwa ikionesha katika ngazi ya kitaifa na kimataifa.
Shughuli za utalii za siku za lavender zahimiza maendeleo ya uchumi katika Mkoa wa Xinjiang, China
Wajenzi waendelea kujenga daraja refu zaidi duniani katika Mkoa wa Guizhou wa China
Majira ya kuvuna mazao ya mpunga yawadia katika Mkoa wa Hainan, Kusini mwa China
Migodi iliyotelekezwa yageuzwa kuwa vivutio vya kitalii katika Mkoa wa Shandong, China
people.cn © Tovuti ya Gazeti la Umma